Sat, 20 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Miamba ya DR Congo,TP Mazembe wakiongozwa na mmiliki wao Moise Katumbi wamehudhuria tena kanisani kwenye ibada maalumu kuelekea mchezo wao wa hatua ya nusu fainali ya Ligi ya mabingwa Afrika dhidi ya klabu ya Al Ahly hii leo.
Ikumbukwe TP Mazembe wamekuwa na utaratibu huu ambapo walifanya hivi pia kwenye mchezo wao wa hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa afrika dhidi ya Petro Atletico ya nchini Angola ambapo walifanikiwa kuwaondosha waangola hao na kutinga nusu fainali.
Mchezo wao dhidi ya Al Ahly utapigwa leo majira ya saa 10:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live