Sun, 25 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
P Mazembe imefuzu kwa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuifunga Pyramids FC ya Misri Jumamosi Februari 24, 2023 kwa ushindi wa mabao 3-0
TP Mazembe maarufu kwa jina la Kunguru wamepata ushindi mkubwa nyumbani, Joël Beya akimalizia pasi ya Glody Likonza dakika ya 32 baadae Glody Likonza akawa mfungaji wa bao la pili, muda mfupi kabla ya mapumziko (45+2′) huku Patient Mwamba akishindilia msumari wa mwisho dakika ya 92.
Wakongo hao wanafuzu kwa robo fainali hata kabla ya siku ya mwisho dhidi ya Mamelodi Sundowns ambapo TP Mazembe ilikuwa haijatinga robo fainali tangu 2020.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live