Wed, 16 Dec 2020
Chanzo: zanzibar24.co.tz
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Vijana Sanaa na Utamaduni Omar Hassan (King) ametaja Orodha ya timu tisa (9) zilizothibitishwa kushiriki katika Mashindano ya Kombe la Mapinduzi 2021 zipo 4 kutokea Zanzibar na 5 kutokea Tanzania bara.
Timu hizo amezitaja wakati alipokua akizungumza na Waandishi wa Habari za Michezo kuhusu Mashindano ya Kombe hilo akiwa huko Ukumbi wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Kikwajuni Jijini Zanzibar.
1. Mlandege. 2. Malindi. 3. Jamhuri. 4. Chipukizi. 5. Simba. 6. Yanga. 7. Namungo. 8. Azam. 9. Mtibwa.
Chanzo: zanzibar24.co.tz