Sat, 16 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Shirikisho la Mpira wa miguu nchini 'TFF' limetangaza kuwa mapato ya mwaka 2023 ni bilioni 40.38 kwa ufafanuzi wa kwamba, bilioni 18.74 zimekusanywa na TFF ilhali bilioni 22.14 zimekusanywa na bodi ya Ligi 'TPLB'.
Vile vile TFF imeelekeza kuwa, makadirio ya bajeti ya matumizi ya mwaka 2024 ni bilioni 41.5 kwa ufafanuzi kwamba, TFF imekadiriwa bilioni 18.02 ilhali bodi ya Ligi ni bilioni 22.13.
Ripoti hiyo ya mapato na matumizi imewasilishwa na Mwakilishi wa Makamu wa kwanza wa Rais wa TFG, Athumani Nyamlani kwenye Mkutano Mkuu wa TFF Jumamosi ya Leo Disemba 16, 2023 mkoani Iringa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live