Tue, 17 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Katika kuhakikisha Serikali inafanikisha ukarabati wa uwanja na Mkapa ili uweze kukidhi vigezo kama walivyotaka CAF, Shirikisho la mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limechangia kwa kuweka viti (Technical Benches Sets) vya kisasa vyenye hadhi ya FIFA.
Viti hivyo vina thamani ya dola 30,000 (sawa na Tsh milioni 75) ili kuhakikisha uwanja wa Mkapa unavutia na unakuwa bora zaidi Afrika.
Hii yote ni kuelekea katika mchezo wa Africa Football League unaoshirikisha timu 8 tu huku mchezo wa ufunguzi ukiwa ni kati ya Mnyama Simba SC Tanzania dhidi ya mabingwa wa Afrika, Al Ahly ya Misri.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live