Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF, linajipanga kuwachukulia hatua Mashabiki wa Klabu ya Simba waliowafanyia vurugu Mashabiki wa Yanga siku ya Jumapili Februari 13 katika Dimba la Mkapa wakati wa mchezo wa Simba .
Aidha TFF imekemea vikali tabia hiyo na kusema kuwa wanakusanya ushahidi wa tukio hilo, kisha hatua madhubuti zitachukuliwa dhidi yao wote waliohusika katika tukio hilo.
Vile vile Shirikisho hilo limetoa tahadhari kwa wale wote wanaotoa shutuma kwa viongozi na maneno ya kuhamasisha vurugu wako mbioni kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa kanuni.
Tazama hapa chini Taarifa kamili ya TFF;