Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

TFF, Simba ni moto unaokolea taratibu

Babra Azuiwa Mtendaji Mkuu wa Simba, Babra Gonzalez

Sat, 11 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Sahau kuhusu msimamo wake wa kutoruhusu timu ya Simba kuvaa Logo ya Mdhamini mwenza Ligi Kuu Bara, GSM, sahau kauli ya Mwenyekiti wake kudai watakwenda kucheza Ligi hata Zanzibar, leo kuna jipya kati ya Mtendaji Mkuu wa Simba na wahusika ndani ya dimba la Mkapa katika mchezo wa Dabi.

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) limefafanua taarifa ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba, Barbara Gonzalez kuzuiwa kuingia kushuhudia timu yake ikicheza dhidi ya Yanga leo uwanja wa Mkapa.

Muda mfupi kabla mechi baina ya Simba na Yanga kuanza, Mtendaji Mkuu wa Simba alisambaza video na kuelezea kuwa amezuiwa kuingia uwanjani na ofisa wa Bodi ya Ligi akiwa na familia yake.

Taarifa iliyotolewa na Ofisa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo baada ya mechi hiyo kumalizika kwa sare tasa, ilieleza kuwa mtendaji huyo alizuiwa kuingia sehemu ya kukaa ya VVIP akiwa na watoto ambao hawaruhusiwi kuingia katika eneo hilo huku wakiwa na kadi za wau wengine walioalikwa kinyume na utaratibu unavyotakiwa.

Hata hivyo, imeelezwa kuwa Barbara yeye aliruhusiwa kuingia na alianza kutoa lugha isiyofaa kwa ofisa huyo huku akirekodi video na baadaye alitupa kadi hizo na kuondoka.

"TFF imesikitishwa na vitendo vya vurugu vilivyofanywa na baadhi ya viongozi wa Simba kwenye eneo la kuingilia Jukwaa la watu maalumu, pia viongozi wengine walifanya vurugu eneo la kuingili baada ya kutakakulazimisha mmoja wa viongozi kuingila bila kadi ya mwaliko," ilieleza taarifa hiyo ya Ndimbo.

Soma kwa undani Taarifa hiyo ya TFF;

Chanzo: www.tanzaniaweb.live