Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

TETESI ZA USAJILI: Vigogo waingia vitani kumuwania Bellingham

Jude Belligham JJ Jude Bellingham

Tue, 21 Mar 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Spurs wanataka pauni milioni 100 mbele kwa mshambuliaji wa Uingereza Harry Kane ikiwa watafikiria kumuuza mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 msimu wa joto wakati atakuwa amebakiza mwaka mmoja kwenye mkataba wake.

Chanzo: [Times - subscription required]

Manchester City wanazidi kujiamini kuwa wanaweza kumpata Muingereza Jude Bellingham, 19, msimu wa joto, lakini Real Madrid wanasalia kwenye mbio za kumnunua kiungo wa kati wa Borussia Dortmund.

Chanzo: [ESPN]

Tajiri mwenye nia ya kuinunua Manchester United (Sir Jim Ratcliffe) anasema hataki kulipa "bei ya kijinga" kwa klabu hiyo.

Chanzo: [Wall Street Journal]

Tottenham Hotspur wanatarajiwa kukubaliana na kuondoka kwa meneja wao Muitaliano Antonio Conte, 53, wiki hii, huku mchezaji wa zamani na kocha wa kikosi cha kwanza Mwingereza Ryan Mason, 31, akitarajiwa kuchukua usukani hadi mwisho wa msimu huu.

Chanzo: [Telegraph - subscription required]

Arsenal wako tayari kumpa mkataba mchezaji wa Norway Martin Odegaard, 24, mkataba mpya wa kumuweka katika klabuni hapo hadi 2030.

Chanzo: [Football Transfers]

Newcastle United inalenga kumlenga kiungo wa Manchester United Scott McTominay msimu huu wa joto na mchezaji huyo wa kimataifa wa Scotland, 26, anaaminika kuwa tayari kuhama.

Chanzo: [Telegraph - subscription required]

Matumaini ya Juventus kumsaini N'Golo Kante, 31, bila malipo msimu wa joto yamekatizwa, huku kiungo huyo wa kati wa Ufaransa akitarajiwa kusaini mkataba mpya wa miaka miwili Chelsea.

Chanzo: [Tuttomercato - in Italian]

Arsenal, Tottenham na West Ham wamemtazama mshambuliaji wa Red Bull Salzburg, Noah Okafor, huku kandarasi ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Uswizi ikikamilika msimu wa joto 2024.

Chanzo: [Daily Mail Sport]

Kipa wa Aston Villa aliyeshinda Kombe la Dunia Emiliano Martinez anasisitiza kuwa anapanga kusalia katika klabu hiyo.

Licha ya kuvutiwa sana na mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 30 kuna Vilabu vinavutiwa na mchezaji huyo.

Chanzo: [Mirror]

Chelsea wako tayari kumuuza mlinda mlango wa Senegal Edouard Mendy, 31, kufuatia kuvunjika kwa mazungumzo ya kuongeza mkataba mpya.

Chanzo: [Football Insider]

Mchezaji wa Fulham ambaye ni kiungo wa kati wa zamani wa Manchester United Andreas Pereira, 27, anavutia Chelsea, ambao wanamwona Mbrazil huyo kama mbadala wa Muingereza Mason Mount, 24 - lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Atletico Madrid na Paris St-Germain.

Chanzo: [ESPN]

Nahodha wa Barcelona Mhispania Sergio Busquets, 34, anafikiria ofa kutoka kwa Ligi Kuu ya Soka ya Saudi Arabia, lakini ataamua wakati wa mapumziko ya kimataifa ikiwa atazikataa au kukubali mkataba mpya wa kusalia Nou Camp.

Chanzo: [Mundo Deportivo - in Spanish]

Chanzo: www.tanzaniaweb.live