Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

TETESI ZA USAJILI: Guardiola amfungia vioo Joao Cancelo

Pep With Joa Cancelo Pep Guardiola na Joao Cancelo

Wed, 26 Jul 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya Nottingham Forest imemsajili Anthony Elanga kwa ada ya pound million £15m kutoka Manchester United kwa mkataba wa miaka 5.

Klabu ya Chelsea imekataa ofa ya kwanza ya West Ham United kwa ajili ya kupata saini ya kiungo Conor Gallagher, pound million £40m plus Add-ons,

Baada ya majadiliano ndani na pia kocha Mauricio Pochettino Chelsea wameamua kukataa ofa hiyo.

West Ham bado wana nia na kiungo huyo, na Chelsea wanataka angalau pound million £50m ili kumuuza Conor Gallagher.

Kocha wa Manchester City Pep Guardiola amtaki João Cancelo katika kikosi chake kuelekea msimu ujao, lakini kwa sasa hakuna njia mbadala wa mchezaji huyo.

Vilabu kadhaa vya Saudi Arabia vimepokelewa na wakala wake Jorge Mendez lakini vimemkataa.

Beki wa kati Igor Julio anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya leo kabla ya kujiunga na Brighton akitokea Fiorentina,

Brighton ilikua inamtaka sana LEVI COLWILL na Chelsea haitaki kumuuza na hii moja ya sababu ya Brighton kuweka ugumu Kwenye uhamusho wa CAICEDO,

Je baada ya kumpata huyu mlinzi watamuachia CAICEDO maana mlengwa wao mkuu alikua Levi Colwill

WATALEGEZA KAMBA ?

Ofa ya £37m ya Liverpool kwa ajili ya kumsajili kiungo wa Southampton Romeu Lavia imekataliwa Southampton wakisisitiza wanaitaji ada ya £50m.

Wakala wa Sadio Mane atasafiri kwenda hadi Japan kwa ajili ya kufanya mazungunzo na Al Nassr,

Wakala wa Sadio Mane atafanya mazungumzo ya kibinafsi na Al Nassr FC baada ya Mane kuruhusu

Mane Alitaka kubakia Bayern Munich kwa hali yoyote ile lakini Bayern wanataka kumuuza.

Mlinda lango wa kimataifa wa Japan Zion Suzuki amekataa ofa ya kwenda kujiunga na klabu ya Manchester United.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live