Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

TETESI ZA USAJILI: Chelsea kuendelea kushusha vyuma kikosini

Teun Koopmeiners Atalanta 2023 2324 1693318824 115299 Teun Koopmeiners

Mon, 15 Apr 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kocha wa zamani wa Bayern Munich, Monaco na Wolfsburg Niko Kovac anaibuka kama jina la kushangaza linalozingatiwa kumrithi Jürgen Klopp kama bosi wa Liverpool.

Newcastle United wamemfanya kiungo mshambuliaji wa Nottingham Forest Mwingereza Morgan Gibbs-White, 24, kuwa mmoja wapo wa walengwa wao wakuu wa uhamisho wa majira ya joto.

Liverpool inaweza kumsajili winga Mwingereza Marcus Edwards, 25, kutoka Sporting Lisbon kwa £30m msimu huu wa joto.

Marcus Rashford anatazamiwa kusalia klabuni Manchester United kwani Paris Saint-Germain wameweka wazi kuwa hawana nia ya kumsajili mshambuliaji huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 26.

Chelsea inatayarisha ofa ya kumnunua kiungo wa kati wa Uholanzi Teun Koopmeiners, 26, baada ya kutuma maskauti kumwangalia wakati Atalanta ipopata Ushindi wa Europa League dhidi ya Liverpool.

Tottenham Hotspur wanamfuatilia kiungo wa kati wa Leicester City Muingereza Kiernan Dewsbury-Hall na wanaweza kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 kati ya £30m au ​​£40m msimu huu wa joto.

Tottenham Hotspur pia ina nia ya kumsajili beki wa Italia Riccardo Calafiori, 21, kutoka Bologna msimu wa joto.

Winga wa Uhispania Bryan Gil anaweza kutaka kuondoka kutoka Tottenham Hotspur msimu wa joto na Spurs itakuwa tayari kumruhusu mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 kuondoka kwa uhamisho wa kudumu.

Everton wana nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Ubelgiji Leander Dendoncker, 28, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Napoli, kutoka Aston Villa msimu huu wa joto.

Barcelona wana uhakika mlinzi wa kati wa Uhispania Pau Cubarsi, 17, atatia saini kandarasi mpya licha ya vilabu vikubwa zaidi vya Ulaya kumtaka.

Barcelona pia wanafanya kazi ya kumuongezea mkataba wa Lamine Yamal, hata kama Paris Saint-Germain itawasilisha nia yao kwa kutoa ofa kubwa kumnunua winga huyo wa Uhispania mwenye umri wa miaka 16.

Bayern Munich wamewasiliana na Zinedine Zidane, ambaye bado hajarejea kwenye uongozi tangu aondoke Real Madrid miaka mitatu iliyopita, imefanya hivyo ili kupima nia yake ya kurithi mikoba ya Thomas Tuchel mwishoni mwa msimu huu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live