Fri, 21 Apr 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kipa namba tatu wa Simba, Ally Salim amesaini mkataba mpya wa miaka mitatu kusalia klabuni hapo hadi 2027 huku akidaiwa kuboreshewa maslahi yake kama njia mojawapo ya kumbakisha kikosini hapo.
Ally Salim ameonekana kufanya vyema katika mechi za hivi karibuni za Simba na kupongezwa na wengi huku akionekana kuziba vyema pengo la Aishi Manula ambae ni majeruhi.
Pambano lililompa sifa zaidi ni dhidi ya Yanga Jumapili iliyopita ambako aliondoka na clean sheet.
Je, una maoni yoyote kwa Mlinda mlango huyo kuongezewa Mkataba?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live