Thu, 17 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mabosi wa Simba katika kuhakikisha wanalisuka benchi la ufundi kuwa imara zaidi ya wakati huu baada ya kumtambulisha kocha wa makipa, Chlouha Zakaria muda wowote kuanzia sasa wanamalizana na chuma kingine.
Taarifa kutoka ndani ya Simba ambazo Mwanaspoti imezipata mabosi wa timu hiyo wamemleta nchini kocha wa viungo kutoka Afrika Kusini ambaye limepatikana jina moja la Kelvin.
Meneja habari wa Simba, Ahmedy Ally alisema: “Siku si nyingi kuna mtaalamu mwingine kwenye benchi la ufundi tutamtambulisha ataungana na waliopo sasa.”
Chanzo: www.tanzaniaweb.live