Taarifa kutoka nchini Afrika Kusini zinaeleza kuwa aliyekuwa kocha mkuu wa wekundu wa Msimbazi Simba SC Pablo Martin yupo mbioni kujiunga na timu ya Amazulu inayoshiriki ligi kuu nchini humo
Kwa mujibu wa mkataba awali uliovuja mitandao ambao bado haujathibitishwa umeonesha kuwa kocha huyo alikuwa ameahidiwa mshahara mnono unaofika milioni 70 za Tanzania kwa mwezi pamoja na mahitaji mengine muhimu.
Baada ya kutoka taarifa za Simba SC kuachana na kocha huyo kutoka Hispania kumezidisha uvumi wa taarifa hii kuwa huenda alichagua kukubali ajira mpya nchini Afrika Kusini.
Pablo hajapatikana kujibu kuhusiana na tetesi hizi.