Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

TETESI: Mayele aomba kuvunja mkataba Pyramids

Mayele MsA Fiston Mayele.

Thu, 29 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mshambuliaji wa zamani wa Klabu ya Yanga, Fiston Mayele amewasilisha barua kwenye Menejiment ya klabu ya Pyramids kwaajili ya kuhitaji kusitishiwa mkataba wake.

Vyombo mbalimbali vya Habari kutoka Misri vimeripoti kuwa Mayele amedai hana furaha kuitumikia zaidi Pyramids FC na ameshafanya mazungumzo na Uongozi wake unaomsimamia ili kupata changamoto nyingine akiondoa Pyramids.

Taarifa za kuaminika ni kuwa Mayele ambaye ni raia wa Congo DR anautaka usimamizi wa Klabu ya Pyramids ya nchini Misri kusitisha mkataba wake.

Taarifa za ndani zinaeleza kuwa, licha ya Simba kuonesha nia, lakini Wauza Ukwaju wa Dar es Salaam, Klabu ya Azam FC wanahusishwa pia katika mipango ya kumsajili Mayele.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: