Fri, 6 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Huku sakata la kiungo Mzanzibari Feisal Salum likiwa halijapatiwa ufumbuzi, inaonekana bado bundi ananyemelea mitaa ya jangwani.
Inadaiwa kuwa Klabu ya Yanga wamempa mkataba mpya mlinzi wa wa kati Dickson Job lakini amegoma kumwaga wino na sababu ni beki huyo kupata Ofa kubwa ktoka klabu za Simba, Azam na timu kutoka Uarabuni.
Yanga imempa mkataba mpya ambao atalipwa mara mbili ya mshahara aliokuwa anaupata na sasa atakuwa anapata ya Sh 4m kitu ambacho Job bado hajakubaliana nacho.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live