Tue, 21 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Huenda kocha Mkuu wa klab ya Al Hilal ya Sudan, raia wa Congo DR, Florent Ibenge tukamshuhudia akikifundisha Kikosi cha Azam Kwa msimu ujao.
Azam ambao wamekuwa wakijitafuta kwa muda mrefu wanaona Kocha huyo ndio mtu sahihi wa kuwafikisha pale ambapo Mabosi wanapahitaji.
Ibenge ana rekodi nzuri Michuano ya CAF Afrika akibeba ubingwa wa Kombe la Shirikisho msimu uliopita akiwa na RS Berkane na msimu huu anapambana kuipeleka Al Hilal hatua ya Robo Fainali Ligi ya Mabingwa Afrika.
Inaelezwa kuwa mazungumzo baina ya pende hizo mbili tayari yameshaanza.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live