Mshambuliaji wa FC Lupopo ya DR Congo, George Mpole ameamua kubadili gia akiwa angani, licha ya kuwa alishakubaliana kila kitu na klabu ya Kitayosce ila sasa akili yake ipo Jangwani.
Siku ya Alhamisi alionekana na Bosi Mkubwa wa klabu ya Yanga huku akionekana mwenye furaha.
Huenda akawa bbadala na Hafiz Konkon ambaye Yanga SC wanazungumzwa kumtaka na huenda wakaamua kuachana nae.
Pia kutua kwa Mpole Yanga Sc inaonyesha kuna mshambuliaji mzawa ataondolewa pale, iwe kutolewa kwa mkopo ama kuvunjiwa Mkataba.
Washambuliaji wa kati (Mambo yakikaa sawa)
Fiston Mayele
Clement Mzize
Kennedy Musonda
Yusuph Athuman
George Mpole