Klabu ya Yanga huenda ikalazimika kuachana na mchezaji wao Chiko Ushindi endapo Benard Morrison atajiunga tena na Yanga.
Uongozi haujaridhishwa na kiwango Cha mchezaji huyo kutoka DRC aliejiunga nao dirisha dogo.
Habari za kuaminika ni kwamba Benard Morrison ameonesha nia ya kuondoka simba sc huku huku akiwa amebakiza miezi miwili tu Katika mkataba wake.
Simba SC haijamuongezea Mkataba na huenda nafas yake ikachukuliwa na mchezaji wa zamani wa Simba Luis Miquison aliejiunga na Al Ahly ambapo hajaonesha kiwango kizuri.
Al Ahly wapo tayari kumtoa kwa mkopo mchezaji huyo sharti tu Simba SC wakubali kumlipa mshahara wake Kamili na stahiki nyengine.