Fri, 10 Jun 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa Klabu ya Azam FC, Mzambia Rodgers Kola, amefiwa na Baba yake Damiano Kola.
Katika taarifa iliyotolewa na klabu ya Azam FC, imesomeka ikimpa pole Mshambuliaji huyo.
"#TANZIA Kwa niaba ya Bodi, viongozi, wafanyakazi na mashabiki wa Azam FC, tunapenda kutuma salamu za rambirambi kwa familia ya mshambuliaji wetu, Rodgers Kola (@king_kola10), baada ya kufiwa na baba yake mzazi, Damiano Kola Senior. Tunamwomba Mwenyezi Mungu, awatie nguvu na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu. R.I.P Mr. Damiano Kola Senior".
Imesomeka sehemu ya taarifa ya Azam FC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live