Fri, 17 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliyekuwa mlinzi wa kati na nahodha wa Taifa Stars Mwaka 1980 Jella Mtagwa amefariki dunia jana Mei 16, 2024 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (Mloganzila) alipokuwa akipatiwa matibabu.
Mchezaji huyo alikuwa sehemu ya manahodha wa kikosi chaTaifa Stars katika fainali za Mataifa Afrika zilizofanyika nchini Nigeria ,amefariki kutokana na ugonjwa wa Kupooza na Moyo.
Picha ya mlinzi huyo imewahi kutumika katika Stemp. Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live