Sat, 16 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa viungo wa timu ya soka ya wanawake ya JKT Queens, Esau Sanu amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Machi 16, 2024.
Katika taarifa iliyotolewa na timu hiyo kupitia mitandao ya kijamii, imesema Esau amefariki katika hospitali ya Lugalo jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.
Endelea kufuatilia Tanzaniaweb habari zaidi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live