Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Szczesny: Juventus Hawakutaka kurudia kosa lile lile

Wojciech Szczesny Juventus Fc 1595847363 44197 Szczesny: Juventus Hawakutaka Kurudia Kosa Lilelile

Wed, 4 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Wojciech Szczesny anasema Juventus walikubali kwamba hawataweza kupoteza dhidi ya Atalanta kitu ambacho hawakuwa wamefanya dhidi ya Sassuolo wiki iliyopita.

Bianconeri walipata pointi moja kwenye Uwanja wa Gewiss jana kwa kupata sare ya 0-0 dhidi ya Atalanta.

“Siku zote tunacheza ili kushinda, hivyo tunapotoka sare, huwa tunapoteza pointi mbili. Nadhani yalikuwa matokeo ya haki hata hivyo, tulicheza vizuri zaidi katika kipindi cha kwanza, walikuwa bora zaidi kipindi cha pili. Wakati fulani, tulielewa hatukupaswa kupoteza mchezo na tuliteseka kidogo katika dakika kumi za mwisho.” Szczesny aliiambia DAZN.

Hili ndilo kosa tulilofanya dhidi ya Sassuolo, ikiwa ni pamoja na Fede Gatti na mimi. Wakati mwingine lazima ukubali kutoa uwezavyo ili kupata pointi, leo tumefanya vizuri zaidi, tunasikitika hatukushinda, lakini kama nilivyosema, ni hatua muhimu dhidi ya timu yenye nguvu. Alisema Mlinda malngo huyo wa zamani wa Arsenal.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Poland aliokoa bao muhimu katika kipindi cha pili, na kuisaidia Juventus kurejea nyumbani na pointi moja mfukoni. Alipoulizwa aliwezaje kuokoa mkwaju wa faulo wa Luis Muriel, Szczesny alisema kuwa hajui lakini ilikuwa ni muhimu kuokoa mpira huo.

Szczesny alisema kuwa anaamini kuna mengi ya kufanya ili kuboresha. Walicheza vyema dhidi ya Lazio katika kipindi cha kwanza, vizuri dhidi ya Udinese katika kipindi cha kwanza, lakini lazima wasimamie mpira vyema. Jana walifanya vizuri kipindi cha kwanza, lakini walibadilisha mfumo kidogo katika kipindi cha pili, kwa hivyo lazima wachukue hatua moja zaidi ili kuwa na ushindani zaidi.

“Ni Septemba tu, sasa tuna derby nzuri na mapumziko ya kimataifa, lakini tunajiandaa kwa mchezo mmoja kwa wakati mmoja.”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live