Mon, 13 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa zamani wa klabu ya Simba Sven Vandenbroeck amesema anavutiwa kufundisha zaidi Afrika Kusini kuliko kurejea nchini kwaajili ya kuifundisha Simba licha ya kuwa anavutiwa pia na klabu hiyo.
Sven ameweka wazi sababu za kuchagua kufundisha Afrika Kusini ni kutokana na kuwepo kwa mazingira mazuri ya kufundishia pamoja na miundo mbinu tofauti na ilivyo kwa Simba.
"Navutiwa kufundisha pote, Simba au klabu moja wapo ya Afrika Kusini lakini Ligi ya Afrika Kusini ina thamani zaidi, na mazingira yake ni mazuri".
Chanzo: www.tanzaniaweb.live