Mbunge wa zamani wa Mbeya Mjini na Mkongwe wa muziki wa Hip Hop Bongo, Joseph Mbilinyi 'Sugu' ametangaza kuisapoti timu ya nyumbani kwao Mbeya City kwa kununua goli kwa shilingi Milioni 1.
Sugu ametangaza jambo hilo kupitia ukurasa wake wa Instagram, ambapo amesema, amefanya hivyo ili kuinusuru timu hiyo isishuke daraja.
"Mbeya City Stand Up!! Timu yetu iko hatarini kushuka daraja, TUSIKUBALI! Tumebakiza mechi 4 na ili kupona inabidi tushinde hata mechi 2 tu… Katika kuhamasisha Wachezaji wetu uwanjani, Mimi nitatoa 1M kwa kila GOLI la USHINDI kwenye mechi zote zilizobaki na mkwanja utaenda kwa Mfungaji…"