Wed, 26 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Luis Suarez yuko tayari kulipa gharama ya mkataba wake ambao umesalia ndani ya klabu ya Gremio ya Brazil ili aweze kuondoka klabuni hapo na kwenda kujiunga na Inter Miami ya nchi Marekani.
Inter Miami ni klabu ambayo rafiki yake wa karibu Lionel Messi amejiunga nayo baada ya kuondoka PSG kama mchezaji huru.
Msimu uliopita Luis Suarez alijiunga na Gremio kwa mkataba wa miaka 2 ambao atapaswa kuutumikia hadi 2024.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live