Mshambuliaji wa Uruguay, Luis Suarez ametangaza kustaafu soka la kimataifa. Akizungumza huku akitokwa na macho katika wakati wa mkutano na wandishi wa habari mjini Montevideo, Uruguay, Suarez mwenye umri wa miaka 37 amethibisha kwamba mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia wa nchi yake dhidi ya Paraguay Septemba 5 utakuwa wa mwisho timu ya taifa.
Fowadi huyo wa zamani wa Liverpool na Barcelona ni mfungaji bora wa muda wote wa Uruguay akiwa na mabao 69 katika michezo 142 akianza kucheza timu ya taifa katika mechi dhidi ya Colombia Februari 2007.
"Nimekuwa nikifikiria na kuchambua hili. Ninaamini huu ndio wakati sahihi," amesema Suarez. Suarez amecheza mishindano 9 makubwa ya kimataifa timu ya ifa Uruguay.