Suala si Steven Gerrard kuwa kocha mkuu wa Aston Villa, bali ni atavuna nini kwa mwaka?
Baada ya kusaini mkataba wa miaka mitatu kama Kocha Mkuu wa Villa, imefahamika kuwa nyota hiyo wa zamani wa Liverpool, atavuma kiasi cha Paundi milioni tano kama malipo ya kibarua chake kipya.
Pesa hizo zinamfanya Gerrard kuwa kocha anayelipwa zaidi katika historia ya makocha wa klabu hiyo.
Baada ya miaka sita kuondoka England kama mchezaji wa Liverpool, Gerrard anarejea tena kama kocha mkuu wa Aston Villa, akichukua nafasi ya Dean Smith ambaye aliondolewa siku nne zilizopota kutokana na matokeo mabovu