Taarifa kutoka Nchini Uganda zinaripoti kuwa Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Uganda (The Cranes) Milutin Sredojević atafutwa kazi endapo atapoteza kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Tanzania ugenini.
Taarifa kutoka Nchini Uganda zinaripoti kuwa Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Uganda (The Cranes) Milutin Sredojević atafutwa kazi endapo atapoteza kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Tanzania ugenini. Uganda wako nchini Tanzania tayari kwa ajili ya mchezo wao wa marudiano utakaopigwa kesho saa 2:00 usiku huku wakiwa na kumbukumbu ya kichapo cha bao 1-0 kwenye mchezo wa awali uliopigwa pale Suez Canal Stadium Jijini Ismailia nchini Misri.