Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Stars mpya ni vita ya makipa

Makipa+pic Stars mpya ni vita ya makipa

Sat, 3 Oct 2020 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

 KOCHA mkuu wa Taifa Stars, Etienne Ndayiragije amepangua safu yote ya ulinzi ya timu hiyo katika uteuzi wa jana kujiandaa na mechi dhidi ya Burundi Jumapili ijayo.

Ettienne alitangaza kikosi cha wachezaji 25 kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa huku mabeki wa kati kukiwa na maingizo mapya wakiwemo Iddi Mobby kutoka Polisi Tanzania na Dickson Job wa Mtibwa Sugar ambao watasaidiana na Bakari Mwamnyeto (Yanga) na Abdallah Sebo wa Azam.

Mchezo huo utapigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam, huku timu hiyo ikiingia kambini keshokutwa Jumatatu.

Aggrey Morris ambaye ameongoza safu ya ulinzi ya Azam kucheza michezo minne ya ligi bila kuruhusu bao hayupo kikosini.

Kuhusu maingizo mapya kama Iddi Mobby, Dickson Job na Abdallah Sebo, Etienne alisema amewaita ili kuwapa uzoefu na kuwaamini.

“Kuna wachezaji wapya nimewajumuisha katika kikosi na ni baada ya kuridhishwa na uwezo wao katika timu zao wakati ligi inaendelea.Ninachoomba tuwape sapoti ili waendelee kujiamini na naamini kabisa wataisaidia timu,”

Chanzo: mwanaspoti.co.tz