Nyota wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars wameahidi kutoa kila walichonacho uwanjani leo ili waweze kuibuka na ushindi katika mechi ya kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2026 dhidi ya Morocco utakaochezwa kuanzia saa 4:00 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.
Nyota wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars wameahidi kutoa kila walichonacho uwanjani leo ili waweze kuibuka na ushindi katika mechi ya kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2026 dhidi ya Morocco utakaochezwa kuanzia saa 4:00 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Ushindi katika mchezo wa leo unaweza kuipeleka Taifa Stars kileleni mwa msimamo wa kundi E ambapo itafikisha pointi sita lakini hiyo itategemea na matokeo ya mchezo baina ya Niger na Zambia.