Sun, 5 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa Timu ya Taifa "Taifa Stars", Kim Poulsen ameita kikosi cha wachezaji 23 ambacho kitaingia kambini kesho kujua saa na mchezo wa kirafiki katika sherehe za miaka 60 ya Uhuru dhidi ya Uganda Desemba 9.
Katika kikosi hicho hajajumuishwa mchezaji hata mmoja wa Simba au Yanga, bila shaka kuziachia fursa klabu hizo ya maandalizi ya pambano baina yao Desemba 11.
Hali kadhalika Simba wao wako kule nchini Zambia walipokwenda kukipiga na Red Arrows mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live