Aliyewahikuwa mchezaji wa Klabu ya Soka ya Manchester United, Phil Mulryne sasa ni padre wa Kanisa Katoliki huko nchini kwao Ireland ya Kaskazini.
Mulryne (45) ambaye amezichezea klabu za, King's Lynn, Leyton Orient, Cardiff City, Norwich City na Manchester United kwa nyakati tofauti, aliamua Kumrejea muumba wake baada ya kuchoshwa na pesa pamoja na wanawake.
Akiwa na miaka 31, mchezaji huyo alistaafu soka la kulipwa wakati huo akiitumikia Norwich City nakuamua kurudi nyumbani kwao.
Baada ya kujitathmini kwa kina, aliona bora akaanza taratibu za kuimarisha imani yake kwa kuwasaidia wasio jiweza na wasio na makazi.