Mchezaji wa ‘klabu’ ya Chelsea, Cole Palmer, amekiri kuwa yeye ni shabiki wa muda mrefu wa ‘klabu’ ya Manchester United, licha ya kuwa anaichezea Chelsea.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 amekiri kuwa licha ya kulelewa katika academy ya Man City, na kuwa mchezaji wa Chelsea, lakini amekuwa shabiki mkubwa wa muda mrefu wa Man United.
Cole Palmer alijiunga na ‘klabu’ ya Chelsea, akitokea Manchester City amekuwa kwenye kiwango bora sana, baada ya kufanikiwa kufunga mabao manne, na kutoa assist mbili, kwenye michezo kumi, hatua iliyomuwezesha kuitwa kwa mara ya kwanza, na ‘kocha’ Gareth Southgate kwenye kikosi cha ‘timu’ ya Taifa ya #England ya wakubwa.