Tue, 22 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa klabu ya Brentford Ivan Toney amesema kama ataondoka klabu ambayo angependa kwenda ni Liverpool kwani amekuwa shabiki wa Liverpool maisha yake yote.
Toney amesema tangu akiwa mtoto alikuwa anaipenda Arsenal, anaiangalia aina ya uchezaji wao na mashabiki wake walivyo na mzuka lakini yeye ni shabiki wa Liverpool na timu hiyo ipo moyoni mwake.
Mchezaji huyo kwa sasa anatumikia adhabu ya kufungiwa miezi 8 kujihusisha na Soka baada ya kukutwa na makosa ya kubashiri.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live