Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Spurs wamgeukia Hakim Ziyech

Ziyech Ushauri Hakim Ziyech

Tue, 11 Apr 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Tottenham Spurs wako mbioni kumsajili winga wa Chelsea Hakim Ziyech msimu huu wa joto baada ya bei ya mchezaji huyo kupunguzwa.

Ziyech hana nafasi Stamford Bridge, hajaichezea The Blues tangu kichapo cha 2-0 kutoka kwa Spurs mnamo Februari. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Morocco mwenye miaka 30, yuko chini ya mkataba hadi 2025, lakini West Londoners wanatarajiwa tu kuomba pauni milioni 20 kwa nambari yao 22.

Spurs, West Ham na Fulham, wanafikiriwa kuwa timu zinazomtaka lakini Paris Saint-Germain wanasalia kuwa wanunuzi zaidi.

Ripoti ya Football Insider PSG itaangalia upya nia yao ya kumnunua mshambuliaji huyo wa zamani wa Ajax baada ya ombi lao la Januari kushindikana dakika za mwisho.

Ziyech ameichezea Chelsea mechi 102 tangu ajiunge nayo mwaka 2020, na kutwaa Ligi ya Mabingwa, Kombe la Super Cup na Kombe la Dunia la Vilabu wakati alipokuwa London Magharibi.

Lakini kuwasili kwa Mykhaylo Mudryk, Raheem Sterling, Noni Madueke na Joao Felix msimu huu kunaonyesha wakuu wa Stamford Bridge wamepoteza imani na mshambuliaji huyo wa Morocco.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live