Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Spurs wafanya kweli EPL

Tottenham Spurs Spurs wafanya kweli EPL

Sat, 28 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ange Postecoglou awatia moyo Tottenham Hot Spurs kuota ndoto zao baada ya timu yake kusonga mbele kwa pointi tano kileleni mwa Ligi kuu kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Crystal Palace jana.

Bao la kujifunga la Joel Ward na mkwaju mwingine wa Heung-Min Son yaliifanya Spurs kuwa mbele kwa mabao mawili katika kipindi cha pili kabla ya Jordan Ayew kufunga bao lao la kufutia machozi.

Kikosi cha Ange Postecoglou kilishikilia bomba hata hivyo, na Mwaustralia huyo alifurahi kusikia mashabiki wao wakiwachangamsha viongozi wa ligi.

Aliiambia Sky Sports: “Wacha wawe na ndoto, hiyo ndiyo maana ya kuwa mfuasi wa soka. Ni sawa kusema kwamba wameteseka kidogo, kwa hivyo sitaweka kizuizi juu ya hilo. Nina furaha sana leo. Hapa ni mahali pagumu kufika na tulilazimika kufanya kazi kwa bidii ili kupata ushindi wetu.”

Kocha huyo anasema kuwa alidhani walikuwa na nidhamu ya kweli na umakini kwa hivyo wamefurahishwa na juhudi walizoweka vijana. Alijua ungekuwa mchezo mgumu kwao.

Palace walitishia muda wote wa mechi na Ange alihifadhi sifa maalum kwa beki Micky van de Ven, ambaye alikuwa muhimu katika kuwazuia wenyeji. Mholanzi huyo ameanza vyema Ligi na bosi wake alisisitiza kwamba yeye ni muhimu kwa mtindo wa uchezaji wa Tottenham.

Meneja wa Spurs alisema: “Jinsi tunavyocheza, tunaihitaji kasi ya Van De Ven. Tunacheza kwa ukali sana na safu yetu na kwa kijana mwenye umri wa miaka 22 ametulia. Inasaidia kuwa na Romero karibu naye, nadhani anajiamini sana kutokana na hilo. Huo ndio uzuri wake.”

Changamoto kwangu ni kwamba hawa jamaa wana mambo mengi zaidi. Ni lazima nihakikishe tunawasukuma na kuwaboresha. Alimaliza hivyo Ange.

Tottenham watarejea uwanjani ndani ya siku 10 watakapomenyana na Chelsea nyumbani.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live