Fri, 12 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Chama cha soka Nchini England (FA) kinapanga kumshawishi mkufunzi Gareth Southgate kuendelea kukinoa kikosi cha England mpaka fainali za kombe la Dunia 2026 bila kujali matokeo ya mchezo wa fainali ya kombe la Mataifa Ulaya EURO 2024 dhidi ya Uhispania siku ya Jumapili.
Mkataba wa sasa wa Southgate unatakatika Mwezi Desemba mwaka huu lakini bosi wa FA, Mark Bullingham anapanga kufanya mazungumzo na kocha huyo baada ya michuano hiyo.
England itakabiliana na Uhispania kwenye fainali za EURO 2024 itakayopigwa siku ya Jumapili Julai 14, 2024 Mjini Berlin Ujerumani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live