Fri, 5 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Yanga, Mahlatse Makudubela ‘Skudu’ na Kocha Miguel Gamond wakiwa kwenye mkutano wa waandishi wa habari kuelekea mechi yao ya kesho dhidi ya Mamelodi Sundowns.
"Tumejiandaa vizuri na tuko tayari kupambana kwa ajili ya timu. Kila atakayepewa nafasi kwenye mechi ya kesho (leo) atajitoa kuhakikisha tunapata matokeo mazuri hapa," amesema Mahlatse Makudubela.
Yanga ipo Afrika Kusini kucheza mchezo wa mkondo wa pili wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Mamelodi hapo leo saa 3:00 usiku.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live