Tue, 9 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Sintofahamu ya aina yake imeibuka kufuatia mchezo wa JKT Queens kushindwa kuanza licha ya awali kufahamika kuwa Olivia upigwe leo Januari 9, 2024 katika Uwanja wa Azam Complex Chamazi jijini Dar.
Hadi muda wa mchezo kuanza ulipowadia majira ya saa 10:00 jioni, walionekana waamuzi wa mchezo huo wakiwa uwanjani na kusalimiana na Simba Queens lakini JKT hawakuonekana.
Taarifa my nyingine zinaeleza JKT Queens walikuwa wakiwasubiri Simba Queens katika Uwanja wao wa Maji General Isamuyo. Bado mpaka sasa haijafahamika nini kipo nyuma ya pazia, na hatma itakuwaje.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live