Mon, 4 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msimu mpya wa Ligi umeanza huku Singida FG wakicheza michezo miwili ya Ligi pasipo kupata ushindi wala kufunga bao lolote.
Mbali na hilo Singida wanajiandaa kucheza mchezo wao wa Mtoano kuwania kufuzu kwa hatua ya Makundi Kombe la Shirikisho.
Bado kiwango chao sio cha kuridhisha huku baadhi ya nyota wao muhimu wakiwa bado wanajitafuta mmojawapo ni Kiungo raia wa Brazil Bruno Gomes.
Singida wanamhitaji huyu mtu arudi kwenye fomu ya kufunga kwa haraka kwa kweli. Bila magoli yake kirahisi wangeikosa nafasi ya 4 msimu uliopita tangu hapo hawafungi magoli mengi na saizi kila mtu miguu mizito.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live