Licha ya kutoanika majina ya wachezaji ilioachana nao kwenye dirisha hili kubwa la usajili, timu ya Fountain Gate imeondokewa na nyota wake muhimu hadi sasa ambao wameonekana kwenye timu nyingine.
Licha ya kutoanika majina ya wachezaji ilioachana nao kwenye dirisha hili kubwa la usajili, timu ya Fountain Gate imeondokewa na nyota wake muhimu hadi sasa ambao wameonekana kwenye timu nyingine. Baada ya viungo, Yusuph Kagoma (Simba) na Aziz Andambwile (Yanga) kusepa wiki hii, nyota wengine wa kikosi cha kwanza, kipa Benedict Haule, mshambuliaji Habib Kyombo na beki wa kushoto, Yahya Mbegu nao wamejiunga na Singida Black Stars na juzi walikuwa sehemu ya kikosi hicho kinachoshiriki michuano ya Kagame.