Klabu ya Singida Fountain Gate, imeweka wazi malengo yao kuelekea msimu ujao wa michuano yote watakayoshiriki msimu wa 2023/24, huku ikishindwa kukunjua makucha yao katika suala zima la kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Вага.
Singida Fountain Gate FC, katika msimu wa 2022/23, ilifanya vizuri kwa kumaliza nafasi ya tatu katika Ligi Kuu hivyo kukata tiketi ya kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika msimu ujao.
Afisa Habari wa Singida Fountain Gate FC, Hassan Masanza, amesema malengo yao ya awali ni kuhakikisha timu hiyo inafanya vizuri katika kila mashindano wanayoshiriki ikiwamo kumaliza nafasi tatu za juu kwenye ligi.