Fri, 19 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Unaambiwa klabu ya Singida Fountain Gate imethibitisha kuachana na aliyekuwa nyota wa klabu hiyo na Mfungaji bora wa Kombe la Mapinduzi "Top straika" Elvis Rupia ambapo wamemtakia kila la heri katika majukumu yake mapya.
Elvis Rupia anakuwa mchezaji wa mwisho kwenye orodha ya wachezaji walioachwa na klabu hiyo ya Singida, na hivyo amehitimisha idadi ya wachezaji 9 waliochwa mwezi huu kwenye klabu hiyo.
Wachezaji wengine walioondoka klabuni hapo ni pamoja na Marouf Tchakei, Medie Kagere, Duke Abuya, Khomeiny, Mukrim Issa, Joash Onyango, Morice Chukwu, pamoja Gadiel Michael.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live