Sun, 28 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Singida Big Stars imejiimarisha kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa kusajili mchezaji mpya, Muargentina, Miguel Escobar.
Klabu ya Singida Big Stars imejiimarisha kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa kusajili mchezaji mpya, Muargentina, Miguel Escobar. Mchezaji huyo anayecheza nafasi ya kiungo mshambuliaji anakuja kuongeza nguvu katika kikosi cha Singida wakati huu ambapo wameanza vyema msimu wa Ligi Kuu Bara wakicheza michezo miwili na kuibuka na ushindi katika michezo yote.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live