Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Singano ashinda kesi dhidi ya TP Mazembe, kuoga noti

SINGANO 1 Ramadhan Singano 'Messi'

Tue, 1 Aug 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ramadhan Singano ameshinda kesi yake dhidi ya TP Mazembe kuhusu malipo yake ya signing fee, ukiukwaji wa vifungu vya kimkataba na mishahara yake, alipata ushindi FIFA ila Mazembe wakaenda CAS ambapo wamebwagwa tena, wanapaswa kumlipa Kijana ndani ya siku 35.

Singano alikuwa na Wanasheria wawili wa kimataifa, kutoka Kenya na Venezuela ambao ndio walisimama kwenye mapambano kwa zaidi ya miaka miwili ya kesi hiyo dhidi ya miamba Mazembe.

Kwasasa rasmi yupo huru ana aweza kujiunga na timu yoyote ile!

Singano amewahi kuvitumikia vilabu kama Azam FC Simba SC, kwa sasa yupo huru alisema

"Kesi yangu imemalizika na sasa nipo huru timu yoyote inayoniitaji tunaweza kuzungumza bado nina kipaji na nina uwezo wa kupambana uwanjani"

Chanzo: www.tanzaniaweb.live