Inaelezwa uongozi wa Simba SC, umeongeza hamasa ya kutafuta ushindi, ambapo kila baada ya ushindi kwenye michezo mitano wachezaji wanapewa Bonus ya shilingi milioni mia moja (Mil.100), ila kwenye michezo mitano ikatokea timu imepata matokeo ya sare au imepoteza basi inaanza upya mpaka pale watakapopata ushindi mfululizo kwenye michezo mitano.
Bonus hii haiondowi Bonus zao zilizopo kwenye mikataba yao kama timu ikishinda au timu ikibeba ubingwa, ambayo wamekubaliana awali kwenye kandarasi zao.
Kwa hiyo Simba SC, ikishinda michezo mitano mfululizo wachezaji pamoja na benchi la ufundi wanapata Bonus mara mbili.