Tue, 15 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
"Tutaendelea kushindania ubingwa mpaka dakika ya mwisho," ni kauli ambayo imetolewa na Kaimu Kocha Mkuu wa Simba SC, Juma Mgunda wakati akizungumza leo kuelekea mchezo wa kesho dhidi ya Namungo.
Simba SC inashika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kuu ikiwa na pointi 21 baada ya kucheza michezo 10.
Ligi hiyo inaongozwa na Yanga yenye pointi 23 akifuatiwa na Azam FC, wenye pointi sawa na Yanga, tofauti ikiwa ni mabao ya kufunga na kufungwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live