Kama masihara lakini wameondoka na alama zote tatu dakika ya mwisho kabisa ya mchezo.
Baada ya piga nikupige ya dakika zote Bull Straika, Meddie Kagere amefunga goli ambalo limeamsha hisia za mashabiki kila pembe ya nchi.
Ndani ya dimba la Mkapa huku wakitawala sehemu kubwa ya mchezo Simba imeondoka kifua mbele baada ya kuichapa Namungo FC kutoka Lindo kwa goli 1-0.
Namungo ambao walikua pungufu baada ya mchezaji wao kuonyeshwa kadi nyekundu dakika za mapema kipindi cha pili na wakajitahidi kucheza kwa nidhamu ya hali ya juu.
#NBCPLUpdates Goli la pointi tatu kutoka kwa Medie Kagere dakika ya mwisho ya mchezo. Hili ni goli lake la pili kwenye ligi msimu huu.
— Azam TV (@azamtvtz) November 3, 2021
FT: Simba 1-0 Namungo. #NBCPL #NBCPremierLeague #NBCPLUpdates #LigiKuuYaNBC #SimbaSC #NamungoFC #SimbaNamungo @SimbaSCTanzania pic.twitter.com/XwsTNYqUnO