Fri, 15 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wekundu wa Msimbazi Simba SC wamemziba mdomo Kagera Sugar kwa kumfunga goli 3-0.
Mechi hiyo ambayo haikuwa na kasi kubwa kama ilivyotarajiwa kutokana na Simba kuonesha kasi kwenye mashindano ya Kimataifa, imepigwa katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar.
Magoli ya Simba yalifungwa na Saido Ntibanzokinza kwa mkwaju wa penalti, Sadio Kanoute aliyeweka kamba kwa kichwa na kisha legendari wa muda wote John Bocco kupigilia msumali wa mwisho akitumia uzembe wa beki aliyepiga mpira mfupi kumrudishia golilipa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live