Mon, 1 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wekundu wa Msimbazi Simba SC,wameanza vizuri mashindano ya Mapinduzi Cup kwa kumtandika JKU 3-1.
Mechi hiyo iliyokuwa na ushindani wa aina yake imepigwa katika Uwanja wa Amaan Visiwani Zanzibar.
Magoli ya Simba yalifungwa na Moses Phiri, Jean Baleke na kinda usajili mpya, Saleh Karabaka.
Goli la kufutia machozi la JKU lilifungwa na Neva Kaboma.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live